Jicho Jipya - Think Anew

Jicho Jipya - Think Anew Jicho Jipya - Think Anew is Swahili name for an Eye (Jicho) while Jipya means New, thus with a Freethinking mind to look and reflect on anything anew

Wandugu, kwa miaka mitatu sasa nimekuwa na safari za kwenda Mahak**ani ambapo nilikuwa na kesi, gazeti lilichukua habari...
01/06/2020

Wandugu, kwa miaka mitatu sasa nimekuwa na safari za kwenda Mahak**ani ambapo nilikuwa na kesi, gazeti lilichukua habari yangu wakaigeuza yao na kuiuza bila ruksa yangu wala kunitambua kwenye maandishi kuwa mimi ndiyo chanzo cha habari hiyo...Sasa kwenye uandishi wa habari hilo ni kosa...
Tabia hii ya waandishi wa habari / wahariri wanaojidhania "wana majina makubwa" mimi nimekuwa mhanga kwa muda mrefu, toka miaka ya 1990s,
Nikaamua kuacha kuandikia magazeti ya Tz..
Mtandao ulipokuwa nikawa naandika kwa nadra mtandaoni...
uandishi wangu ni wa kifalsafa zaidi, na kiuchunguzi, na kiurasini - mantiki, siyo siasa, itikadi wala dini k**a ilivyozoeleka Tz.
Lakini hata huko jamaa wakachukua habari yangu na kuigeuza yao...
Nilipowauliza kunani? hawakunijibu, jeuri ya ulimbukeni, ya kuyakuta maisha ya middle class ukubwani..!
Nikawauliza tena wandugu vipi..? Wala hawakutaka kuniona...dhalau kwani nitawafanya nini? Who is Nsajigwa? Si ni jamaa tu wa mtaani..?
Sasa nikawa na option mbili, aidha "nimuachie Mungu" k**a ilivyozoeleka au nijipiganie mwenyewe kwa akili zangu, potelea mbali matokeo yoyote, kwa kuwa mimi ni freethinker kwa falsafa ya maisha yangu, suala la "kumuachia mungu" halipo...
Ikabidi tu niwapeleke mahak**ani, nikajisimamia mwenyewe kesi bila wakili, nikisaidiwa na kaka mdogo (sasa ndugu yangu) mwanafunzi tu wa sheria (wao waliweka wakili, ni gharama sana kuweka wakili, yabidi umlipe kila anapokwenda mahak**ani, kwa kesi inayoendelea muda mrefu unaweza ishia njiani ukafilisika kwa madeni)...
Hayo hapo chini ni matokeo ya kesi hiyo, dharau ni mbaya, ulimbukeni ni tatizo...wangekubali tu tuonane wakakubali kosa lao tusingefikishana huko...
Matokeo ya kesi yalikuwa mei /14/2020 wiki mbili zimepita. Nilikuwa kimya mpaka rafiki yangu kijana mwingine mwandishi alipojua hili na kuniambia kaka litoke public, ili iwe fundisho kwa jamii...
Kisheria jamaa wanaweza kukata rufaa, inaruhusiwa, na ikiwa hivyo kesi itahamia Mahak**a ya juu zaidi.
K**a nilivyokwisha amua, nitajipigania mimi mwenyewe mpaka akili yangu ya mwisho...siogopi kwenda Mahak**ani wala siogopi kulumbana kisheria na mawakili, mimi elimu falsafa, lojiki, urasini mantiki, kujiuliza maswali muda wote na kuutafuta na kuuonyesha ushaidi hivyo vyatosha, na hata sheria, nililazimika kusoma vitabu vyao ili kujua kanuni za msingi zinazoendesha kesi, hizi za civil, k**a vile ilivyo kwamba hata k**a hujawahi kucheza soka au mchezo wa bao au chess, unapouangalia utauelewa vizuri pale unapojua sheria na kanuni zake.
Hakika siku za mbeleni natia nia ya kuandika juu ya uzoefu wa kwenda Mahak**ani, nimeyakuta mengi huko...
Freethinker FearlessThinker Fikrahuru Nsajigwa Nsa'Sam MWASOKWA

  an outspoken voice against Boko Haram ideologyMubarak Bala aachiwe huru, ni sauti jasiri dhidi ya itikadi ya imani kal...
07/05/2020

an outspoken voice against Boko Haram ideology

Mubarak Bala aachiwe huru, ni sauti jasiri dhidi ya itikadi ya imani kali ya Boko Haram

06/05/2020

Imani ikizidi inaondoa uhalisia...tatizo viongozi hawa "wa kiroho" wanaaminisha wafuasi wao ujasiri wa kuweza kufanya wasiyoweza...ni sawa na kuvuka mto wenye mamba kwa ujasiri bila kuchukua tahadhali...hivi ukiwa kwenye ndege wakikwambia funga mkanda ikiwa wewe ni muumini wa dini utakataa na kusema unamtegemea mungu tu..?
Abiria chunga mzigo wako, mhubiriwa uwe makini, tumia akili yako pia, huyo mungu (k**a yupo) hata wewe anakuona, kakupa akili, usitegemee za mwingine muda wote, hata akiwa ni kiongozi wako, yeye pia ni binadamu tu, una uhakika gani wa mia kwa mia kuwa yupo sawa muda wote..?
https://m.facebook.com/story.php?story_fbid=2966855910049517&id=100001754101171

06/05/2020

Pitia tafsiri kwa Ki-Swahili, "Tumbua uzushi" kuhusu Corona.
By Nsajigwa Nsa'sam

Hadithi ya corona 2020, wapo wapi wale "manabii" waombeaji wenye "nguvu za kiroho" za kuponya, na waganga wa "ramli" wal...
25/04/2020

Hadithi ya corona 2020, wapo wapi wale "manabii" waombeaji wenye "nguvu za kiroho" za kuponya, na waganga wa "ramli" waliokuwa wanajinadi kutibu "magonjwa yote" mbalimbali..?
Kwanini kesho wewe uwa amini tena..?
Akili mu kichwa mwanamboka wa inchi hii..!

29/10/2019

KIPANDE KUTOKA HOTUBA YA MWALIMU JK NYERERE 23-05-1988,
MWENYEKITI WA CCM TAIFA, ALIPOKUWA ANAJIBU MASWALI YA SEMINA
YA VYOMBO VYA HABARI
Kwa majibu haya chini, swali lilikuwa juu ya dalili za kuibuka udini Tanzania.
Majibu ya Mwalimu Nyerere yalikuwa ifuatavyo:- “Ma Atheist wapo lakini hawasumbui, sijui k**a wanaweza kuandamana, pengine. Wengine wapo kwenye chama.Wanaosumbua ni hawa wenye dini kubwa – Uislamu na Ukristo. Traditionalists nao..? Jehovah witness ni Wakorofi. Kuna madhehebu hawataki kulima tumbaku. Kuna madhehebu hawataki kupeleka wagonjwa hospitali. Hawataki organised govermment.Wapo waislamu wenye matatizo, lakini ni individual si wote, ni mmoja mmoja. Wakristo na Waislamu. Wasio na dini nani? Sijui k**a wanatusumbua sana, labda katika CCM. Sijui k**a wanafanya maandamano. Wa chini ya miembe hawana matatizo. Kichwa maji mkristo aliandika barua ya ovyo sana”...
NB: Hotuba ni k**a ilivyoandika (kaririwa) na Nsajigwa Nsa'sam Mwasokwa, wakati
akisikiliza hotuba ya Tape za Mwalimu Nyerere ktk usaidizi wa ukarimani wa utafiti wa
PhD.

Tanzanian Freethinkers Jichojipya-Think anew meeting on 15th june 2019 in Dar es salaam, it was success...Mkutano wa Wan...
18/06/2019

Tanzanian Freethinkers Jichojipya-Think anew meeting on 15th june 2019 in Dar es salaam, it was success...

Mkutano wa WanafikraHuru huru wa Tz, wale k**a Kingunge kifalsafa, Maadili bila dini uliofanyika 15 june 2019 Dar es salaam, ulifana...

16/05/2019

Maadili bila dini inawezekana?
Mjumuiko wa WanaFikrahuru wa Tz, wale K**a Kingunge june 15 2019
Tupo wachache lakini tupo aisee!

Address

Dar Es Salaam

Telephone

+255714437643

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jicho Jipya - Think Anew posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jicho Jipya - Think Anew:

Share